Maandamano ya amani
yaliyofanyika mjini Mtwara siku ya alhamis wiki hii yameibua hoja mbali mbali
kutoka kwa viongozi, wananchi, vyombo vya habari na mjadala wa siku nzima
kwenye mitandao ya kijamii hasa facebook, twitter na JamiiForums. Mkuu wa Mkoa
wa Mtwara ameita waandamanaji wapuuzi na Waziri wa Nishati na Madini amewaita
watu hatari na
Maandamano ya amani
yaliyofanyika mjini Mtwara siku ya alhamis wiki hii yameibua hoja mbali mbali
kutoka kwa viongozi, wananchi, vyombo vya habari na mjadala wa siku nzima
kwenye mitandao ya kijamii hasa facebook, twitter na JamiiForums. Mkuu wa Mkoa
wa Mtwara ameita waandamanaji wapuuzi na Waziri wa Nishati na Madini amewaita
watu hatari na wahaini. CHADEMA tumetoa kauli kupitia kwa Waziri Kivuli wa
Nishati na Madini kwamba udhaifu wa utendaji serikalini ndio chanzo cha
maandamano haya.
Lakini kuna tatizo
kubwa zaidi ambalo linaonekana siyo katika sekta hii tu bali pia katika sekta
nyingine ambapo tunaona matokeo yake katika maisha ya watu wetu na naweza
kusema ni dalili za kushindikana kwa sera za CCM. Sera hizi ndizo ambazo
zimelifikisha taifa hili hadi hapa. Kama hadi wananchi wa Mtwara ambako kwa
muda mrefu imekuwa ni ngombe ya CCM wanaanza kuhoji matokeo ya sera za chama
tawala basi ni dalili kuwa Watanzania wamefungua macho yao na wanaona.
Wanaona katika
nishati, wanaona katika utawala bora, wanaona katia elimu (kuanzia ya msingi
hadi ya juu kabisa!), wanaona katika afya, wanaona katika utendaji wa jeshi la
polisi wanaona katika madini. Sera za CCM zimeshindwa. Zimeshindwa kuinua
maisha yao na zinaonekana kuendelea kushindwa.
Mtwara na Lindi wanataka nini?
Watu wa Mtwara
wanataka gesi isiondoke Mtwara na badala yake viwanda na mitambo ijengwe Mtwara
kisha kama ni umeme au mbolea isafirishwe kupelekwa sehemu nyingine ya nchi.
Watu wa Mtwara hawasemi kwamba Gesi yote na mazao yake vibaki Mtwara na Lindi.
Wanasema umeme uzalishwe Mtwara usambazwe nchi nzima. Mbolea izalishwe Mtwara
na kusambazwa nchi nzima. Wanataka Bandari ya Mtwara iboreshwe na kuhudumia
mikoa ya Kusini. Watu wa Mtwara hawasemi kwamba mapato yote ya Gesi yatumike
Mtwara tu la hasha.
No comments:
Post a Comment