Rais wa zamani wa Zanzibar ambaye amemaliza muda wake kama makamu
mwenyekiti wa chama tawala nchini CCM hapo jana (13.11.2012) Amani Abeid
Karume amejivunia mafanikio aliyosimamia visiwani humo wakati wa
utawala wake.
Akizungumza na Aboubakary Liongo muda mfupi kabla ya kumalizika kwa
mkutano mkuu wa chama hicho cha CCM mjini Dodoma jana, Amani Karume
amesema kuwa serikali ya umoja wa kitaifa na hali ya amani iliyokuwepo
ni vitu anavyojivunia.(Kusikiliza mazungumzo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)
Mwandishi: Amina Abubaka
No comments:
Post a Comment